Friday, October 11, 2013

HIKI NDICHO ALICHOKIFANYA MSANII YOUNG KILLER JANA

Mkali wa Hip Hop anayewakilisha jiji lenye miamba mingi Mwanza,Young Killer Msodoki amefunguka na kusema kuwa ametimiza ndoto yake jana baada ya kufanya kazi na Msanii mkongwe katika Fani ya Bongo Fleva Dully Sykes.


Killer amefunguka na kusema kuwa Dully skyes ni msanii aliyekuwa anamkubali na kumshabikia tangu zamani wakati hajui kama atakuja kuimba. 
 
Kazi zimefanyika ndani ya studio ya 4:12 ya Dully Sykes na kutayarishwa na Dully mwenyewe.

Kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa kuwa ndiye muweza wa yote, jana tulikuwa na project yetu na Dully, kwanza kabisa picha linaanza mimi ni shabiki mkubwa sana wa Dully. Dully kaanza muziki wakati niko shuleni na sijui hili wala lile, kwa hiyo nilikuwa na dream kubwa sana kuja kufanya kazi na bro Dully na jana bahati nzuri mwenyezi Mungu amebariki tumefanya kazi, haijalishi kama itatoka leo au kesho..na sidhani kama itaishia kazi hiyo, tunaweza kufanya kazi nyingi na nyingi zaidi.” Amefunguka Young Killer.

0 comments:

Post a Comment