Tuesday, September 17, 2013

HUYU NDIE MWANAMKE ANAEISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI KWA ZAIDI YA MIAKA 20 ATOA SIRI YA KUISHI MIAKA MINGI NA VIRUSI VYA UKIMWI.

Nilibainika kuwa naugua ugonjwa wa Ukimwi mwaka 1988 wakati huo nikiwa na umri wa miaka 34. Lakini, nimeweza kuishi salama hadi sasa kutokana na kuzingatia masharti,” hii ni kauli ya Pelagia Katunzi anayeishi na virusi vya Ukimwi (VVU).


Katunzi ambaye sasa ana umri wa miaka 58, anasema mume wake alikufa mwishoni mwa mwaka 1988, baada ya kupimwa na kugundulika kuwa ana ugonjwa huo.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa, wakati huo hazikuwepo dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi na kuchangia kasi ya kifo chake.
baada ya kufahamu hali yake aliishi kwa kuzingatia masharti ya kitaalamu ikiwamo kula chakula sahihi, kutofanya ngono holela hasa ngono zembe, kudhibiti hofu na kutokunywa pombe.

Pia anasema alikuwa muwazi kwa kila mwanaume aliyemtaka kimapenzi alimfahamisha ukweli na hivyo kupunguza msongamano wa wanaume waliokuwa wakimfuata na kumtaka awe na mahusiano nao ya kimapenzi.

Watu wengi wanakufa haraka kwa sababu ya kuwa na hofu, unapojitambua ukaweza kudhibiti hofu unaishi muda mrefu bila kuugua.Lakini, ukiwa na hofu kila wakati, unaugua kila mara na kufa haraka,” anasema.

Mama huyo ambaye wakati mume wake anafariki alimwachia watoto wanne ambao amewalea mwenyewe.

Anasema katika kipindi hicho, alikuwa mdogo, mzuri, anavutia hivyo kama asingekuwa muwazi angeambukiza watu wengi, lakini pia naye angekufa haraka na kuacha watoto wake wakiwa wadogo.

Katika kipindi kirefu anasema kuwa hakutumia dawa bali alizingatia masharti hayo ya kitaalam na kuanza kutumia dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi (ARVs) mwaka 2009.

0 comments:

Post a Comment