Kampuni
ya ndege ya Fastjet inayoaminikia kuwa na huduma ya bei nafuu
Tanzania imekwama kufikia malengo ya kusafirisha abiria kutoka
Tanzania kuelekea Afrika Kusini leo.
Kwa
mujibu wa Taarifa zilizotolewa na Kampuni hiyo ya Fastjet awali
walidai kuwa wangeaanza Kusafirisha abiria kutoka Tanzania na
kuelekaea Afrika Kusini siku ya leo lakini kabla hata ya kuanza kwa
safari hiyo jana abiria ambao walishakuwa wamelipia safari hiyo
walipigiwa simu na kampuni hiyo ili wakachukue pesa zao baada ya
kushindwa kufanya safari hiyo.
Mpaka
sasa hakuna abiria au taarifa zozote zilizotolewa na Kampuni hiyo na
kueleza sababu kuu za kuahirisha safari hizo kwa muda usiojulikana.
Katika
historia hii ni mara ya pili kwa kampuni ya FastJet kushindwa kuanza
safari za Afrika Kusini mara ya kwanza kampuni hiyo ilishindwa kuanza
safari za kwenda nchini humo baada ya kushindwa kutoa malipo ya awali
kwa ajili ya kukodi ndege aina ya Boeing 737 - 300 iliyopanga
kuitumia kwa safari za Cape Town - Johannesbur.







0 comments:
Post a Comment