Monday, July 22, 2013

SIFIKIRI TENA KUCHEZA SOKA TANZANIA- AMRI KIEMBE

Kiungo mwenye kiwango cha juu katika Soka la Bongo achezaye timu ya soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Amri Kiemba, amesema kwamba
hafikirii kurejea Yanga wala timu nyingine yoyote nchini kwani malengo yake sasa ni kucheza soka la kulipwa barani Ulaya na kwingineko nje ya Tanzania.

Uongozi wa Simba kupitia mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage, umetangaza kuwa wamepokea 'ofa' kutoka klabu moja ya Uturuki ikimuhitaji kiungo huyo kwa dau ya dola za Marekani 240,000 (Sh. milioni 379) na kupewa mshahara wa dola za Marekani 15,000 (Sh. milioni 24) kwa mwezi.

" Kwa sasa nawaza kucheza nje ya nchi na sitakataa ofa nitakayoipata," alisema Kiemba.

0 comments:

Post a Comment