Wednesday, July 24, 2013

NYOTA YAKO LEO JUMATANO TAREHE 24/7/2013

SIMBA - LEO (JUL 23 –AUG 22)
Unaonekana kupenda kazi yako lakini hakuna anayejali unayoyafanya, yupo usiyemtarajia atakuja na jibu zuri kwako.

MASHUKE - VIRGO (AUG 23- SEPT 23)
Weka msisitizo zaidi katika yale unayotarajia kuyapanga wakati huu, kuna faida kubwa iko mbele yako, maisha yanaweza kubadilika

MIZANI - LIBRA (SEPT 24- OCT 23)
Masuala ya pesa yatakuingiza kwenye wakati mgumu leo hii, weka mikakati mipya ya kuziba mapengo yatakayotokea.

NGE - SCORPIO (OCT 24- NOV 22)
Kutofanya lolote na badala yake kuangalia mambo yanavyokwenda leo hii ni jambo zuri sana na la maana kwa upande wako

MSHALE - SAGITARIUS ( NOV 23 - DES 21)
Jumatano ya leo yale Yanayosemwa yatakuingiza matatizoni kama utaendelea kuyasikiliza, si kila jambo linaweza kuwa na maana kwako.

MBUZI - CAPRICORN (DES 22 – JAN 20)
Mahusiano yako yatajengwa namna unavyotaka, usikubali ushawishi usioweza kuutekeleza, vinginevyo ni bora kuacha.

NDOO –AQUARIUS (JAN 21 – FEBR 19)
Yanayoendelea kutokea kwa sasa yasikunyime nafasi ya kufanya maamuzi, kila jambo litakwenda kama unavyotarajia.

SAMAKI – PISCES (FEB 20- MACH 20)
Usikubali kupokea ushauri kutoka kwa wengine, ndio nafasi yako ya kusonga mbele, usidharau hata wale usiowategemea.

PUNDA- ARIES (MACH 21- APR 20)
Utahitaji busara badala ya nguvu ili kumaliza tofauti na mwenzako, usipokuwa makini utakaribisha matatizo zaidi,

NG’OMBE – TAURUS (APR21 – MAY 20)
Hutapata shida kama utaanzisha mahusiano aidha ya kikazi au ya kimapenzi kwa siku ya leo, kama hujiamini ni bora kuendeleza na msimamo wako.

MAPACHA - GEMINI (MAY 21- JUN 21)
Wengine wanaweza kukuangalia vibaya lakini hilo lisikupe wasiwasi endelea na msimamo wako na kila jambo litafanikiwa.

KAA - CANCER (JUN 22- JUL 22)
Leo ni jumatano nzuri sana kwako mambo yako mengi yatatengamaa na kujikuta uikamilisha kila jamo lako pamoja na kwamba utapata mapingamizi ya hapa na pale.

0 comments:

Post a Comment