Wednesday, July 10, 2013

MAFUTA YA KULA YAPIGWA MARUFUKU NCHINI NI HATARI KWA WATUMIAJI.



Shirika la Viwango (TBS) limepiga marufuku uuzaji, ununuzi na matumizi ya mafuta ya kula ya aina ya Oki, Viking na Asma baada ya kubainika kuwa hayana ubora na hatari kwa afya za watumiaji.

Kwa mujibu wa Tangazo lilitolewa na Shirika la Viwango nchini (TBS)
kwa baadhi ya vyombo vya habari jana, yeyote atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Viwango Na. 2 ya mwaka 2009.

Tangazo hilo lilisema TBS ilinunua mafuta hayo yanayozalishwa nchini Malayasia na kuingizwa kupitia njia za panya, kusambazwa sokoni na kubainika kuwa hayajakidhi matakwa ya kiwango cha kimataifa kinachotumiwa nchini.

“Matokeo ya uchunguzi wa  sampuli  zake  yalibainika kuwa yameshaharibika kabla ya kufikia ukomo wa matumizi kutokana na kutosafishwa ipasavyo, ni  machafu kutokana na kuchanganyika na maji hivyo  vigezo vya ubora wa mafuta havikufikiwa.”

Kwa msingi huo, TBS imewataka wauzaji wa mafuta hayo  kuyaondoa sokoni  mara moja na wateja kuacha kuyanunua hadi hapo itakapothibitika kuwa yamefikia kiwango kinachotakiwa.

0 comments:

Post a Comment