Wednesday, July 10, 2013

HAPA MZEE MAJUTO PALE JB KWELI “SHIKAMOO”


Wakali wa Filamu Bongo wanaofanya poa sana katika Tasnia hiyo namzungumzia Mzee King Majuto na Mwanae kikazi JB ambao awali walifanya kazi na kuwabamba watu wengi kutokana na Swaga za Mzee Majuto na JB katika kazi hiyo iliyokwenda kwa jina la Nakwenda kwa
Mwanangu’, akimshirikisha gwiji,‘King Majuto’ wajipanga kuja na Shikamoo Mzee

Siku za karibuni Mtayarishaji na muigizaji Jacob Stephen aliingiza sokoni kazi yake iliyokwenda kwa jina la Zawadi  Yangu inayoendelea kukimbiza sokoni kwa sasa, muigizaji nyota  wa filamu nchini, Jacob Stephen 'JB' yupo mbioni kuachia kazi nyingine iitwayo 'Shikamoo Mzee'.

JB alisema kuwa filamu hiyo imewashikirikisha wasanii nyota kama Chuma Suleiman 'Bi Hindu', Amri Athuman 'King Majuto' na Shamsa Ford.

"Baada ya kuwapa mashabiki wangu 'Zawadi Yangu' safari hii wajiandae kupata burudani nyingine  kupitia 'Shikamoo Mzee' ambayo nimeigiza tena na King Majuto, Bi Hindu na wakali wengine,"  alisema JB.

0 comments:

Post a Comment