Wednesday, July 10, 2013

SIMBA ITAKUWA BORA KWA KUMPATA MFUNGAJI BORA?


Hili ni swali ninalo jiuliza kama ambavyo watu wengi wenye mtizamo kama wangu wanavyojiuliza swali hili, Jana usiku Mshambuliaji ambae ni tegemeo wa Mabingwa wa ligi Kuu ya soka kutoka Burundi katika timu ya Vital'O, ametua Tanzania kufanya mazungumzo na kujiunga na Club ya Simba Sports.


Tambwe ambaye aliibuka mfungaji bora katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) kwa kufunga magoli sita na kuisaidia timu yake kutwaa ubingwa wa kwanza wa michuano hiyo, atasaini mkataba wa miaka miwili katika Club ya Simba.

Sinahofu na kiwango cha Mchezaji huyu lakini najiuliza ujio wa Tambwe Msimbazi utaleta Uzima na ufufuo katika Club hiyo?

Simba Sports Club msimu uliopita ilimaliza ikiwa ya tatu na kukosa tiketi ya kushiriki mashindano ya kimataifa mwakani.

0 comments:

Post a Comment