Friday, July 12, 2013

BADO NAMPENDA P-FUNK KWA KUWA NI BABA WA MWANANGU-KAJALA MASANJA


Msanii wa Tasnia ya Filamu Nchini Kajala Masanja ambae siku za karibuni aliachiwa huru dhidi ya kesdi iliyokuwa ikimkabili yeye na mumewe baada ya kupewa Support na Mwadada Wema Sepetu amefunguka na kusema kuwa hana mahusiano yoyote yale na Peti Man na kusema kuwa ni mtu wake wa karibu sana.

Kajala amefunguka hayo leo...........
alipokuwa akichat na Fans wake katika KIKAANGONI LIVE CHAT inayoendeshwa na East Africa Television kupitia ukurasa wake wa Facebook ambapo Fans wanapewa nafasi kuuliza jambo na yeye kulijibu.

Mbali na kukanusha tetesi hizo kuwa anatoka na Peti Man ameeleza kuwa yeye bado ni mke halali wa Faraja Chambo kwa kuwa walifunga ndoa hivyo kinachoweza kuwatenganisha ni Kifo tu na si jambo jingine kwa misingi na imani ya dini.

AELEZEA MAHUSIANO YAKE NA WEMA.
Fans wengi walikuwa wakitaka kujuwa mahusiano yake yeye na Wema Sepetu kwa sasa na hili limekuja baada ya tetesi kuvuma kuwa hawana mahusiano mazuri na Wema Sepetu ambaye ndiye aliingia mfukoni mwake na kutoa pesa kwa lengo la kumuokowa kutofungwa Jela.

Kajala alisema kuwa kwa sasa hawana Tofauti yoyote ile na Wema kwani kila kitu kimewekwa sawa na tofauti zimekwisha kwa maaana hiyo ni poa sana tu.

UPENDO WAKE KWA P-FUNK
Kama kawida unapokuwa mtu maarufu watu huitaji kujuwa mambo yako mmoja kati ya wadau aliuliza swali kuwa Bado unampenda P-Funk Majani? Bila woga mwadada Kajala akasema kuwa bado anampenda P-Funk Majani kwa kuwa ni Baba wa Mtoto wake kipenzi Paula.

0 comments:

Post a Comment