Kaimu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Juma Yusuph, alisema mwanamke huyo
alikamatwa juzi, saa 3.00 usiku, wilayani humo.
Alisema
alipohojiwa, mwanamke huyo alikiri kuwa mtoto huyo si wake na kwamba,
alimpata katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam.
Kamanda
Yusuph alisema mwanamke huyo alidai kuwa yeye hana mtoto na
alikubaliana na daktari hospitalini hapo kuwa iwapo mtu atajifungua,
atamwibia mtoto na kumpa amlee.
Alisema
hata hivyo, hakumtaja daktari huyo kwa madai kwamba, hajui jina lake
na anapoishi.







0 comments:
Post a Comment