Kiungo
mchezeshaji kutoka nchini Rwanda Haruna Niyonzima amesema kuwa yanga
ndio nyumbani kwake na si timu nyingine kwani aichezeapo Yanga huwa
anakuwa na furaha na kuwa malengo yake ni kuisaidia timu hiyo kuweza
kufanya vizuri zaidi katika mashindano mbalimbali.
Niyonzima
amesema hayo leo alipokuwa akisaini mkataba wa miaka miwili na Club
hiyo ya Yanga
“Nawashukuru
wanachama, washabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga kwa kuwa naye muda
wote, Yanga ni nyumbani kwangu kwani najisikia furaha kuichezea timu
hii na malengo yangu ni kuisadia ili iweze kufanya vizuri katika
upatashindano ya kimataifa”
Akiongea
na waandishi wa habari makao ya klabu ya Yanga, katibu mkuu Lawrence
Mwalusako amesema wameamua kumuongezea mkataba mchezaji huyo kufuatia
kuuhitaji mchango wake kwani katika kipindi chake cha miaka miwili
ameonyesha kiwango cha hali ya juu na kutoa mchango mkubwa.
“kumekua
yakiongelewa mengi juu ya mchezaji wetu Niyonzima, baadhi ya vyombo
vya habari vimekua vikitoa taarifa za kupotosha juu yake ukweli leo
umedhihirika kwamba Niyonzima ni mchezaji wa Yanga na ataendelea
kuitumikia kwa miaka miwili”
Haruna
Niyonzima alijiunga na Yanga kwa mara ya kwanza Julai 2011 akitokea
katika timu ya APR nchini Rwanda ambapo katika miaka yake miwili
aliyoichezea timu ya Yanga amefanikiwa kuisadia kupata makombe mawili
ya ubingwa wa Ligi Kuu 2012-2013 na Kombe la Kagame 2011-2012.
0 comments:
Post a Comment