Wednesday, April 10, 2013

NANCY SUMARI AZUNGUMZIA "NYOTA YAKO"

Miss Tanzania aliewahi kushinda Miss World Africa mwaka 2005 Nancy Sumari ameeleza sababu zilizomsukuma kuandika Kitabu Cha Nyota yako alichokiandika kwa lengo la kuwafunza Wanafunzi kujifunza katika watu waliowazunguka katika maisha yao ya kila siku.

Nancy amesema kuwa alipopata mtoto wake wa kwanza ndipo alipata msukumo wa kuona anafanya jambo litakalo wajengea watoto uwezo wa kujifunza kutoka kwa watu wanaowazunguka katika maisha ya kila siku.

Mbali na malengo ya kutunga kitabu ambayo kwa asilimia kubwa ameyafikia lakini lengo kwa sasa ni kuona watu,watoto pamoja na wanafunzi wanakuwa na utamaduni wa kujisomea Vitabu,hivyo atakuwa akifanya Usomaji shirikishi kwa kuzunguka shule tofauti tofauti na kusoma na wanafunzi pamoja lengo kuu ni kujenga utamaduni wa kujisomea kwa wanafunzi ili wajifunze mengi zaidi.

Nacy aliendelea kusema kuwa katika watu waliofanikisha yeye kufikia lengo la kuandika Kitabu hicho ni Mwandishi Shabani Robert kwani anapenda sana uandishi wake na kupenda kazi zake zilizo mpa mwanga yeye kufikia Malengo hayo.

0 comments:

Post a Comment