Thursday, April 11, 2013

KANUMBA ALITUMIA KISWAHILI NA KUFANIKIWA KIMATAIFA

Meneja na Mtayarishaji wa Filamu katika nchi mbalimbali za Africa Prince Richard Nwaobi aliekuwa akisimamia kazi za Marehemu Steven Kanumba amewataka wasanii wengine wa Filamu Tanzania kuondokana na Fikra potofu kuwa Lugha ya Kiiingereza ni tatizo katika soko la Filamu kimataifa.

Meneja huyo aliyasema hayo siku ya maazimisho ya mwaka mmoja toka kufariki kwa Msanii Kanumba,aliwapa mfano wasanii hao kuwa hata Kanumba aliweza kufanikiwa kufanya vizuri kimataifa kwa lugha yake nzuri ya kiwsahili na sii kiengereza kama ambavyo dhana hiyo imewaka wasanii wengi na kuwafanya kuwa waoga kujalibu kufunga katika soko la kimataifa.

Aliendelea kusema kuwa amejitaidi sana kudhuru Tanzania kwa lengo la kutengeneza umoja kati ya wasanii wa Tanzania na Nchi zingine ili kuweza kuteka soko la kimataifa lakini mwamko kwa wasanii kutoka Tanzania umekuwa ni mdogo mnoo ukilinganisha na jitihada alizokuwa nazo Marehemu Kanumba katika Kufikia malengo ya kufanya kazi Kimataifa.

Wasanii wa Tanzania hawawezi kufuata nyayo za marehemu Kanumba kwa sababu wanahofu ya kutojua Lugha ya Kiingereza hawatambui kuna wasanii maarufu wengi ulimwenguni hawajui Kiingereza kabsaaa lakini wanafanya kazi ya sanaa na kufanikiwa duniani pasipo kutumia lugha ya kiingereza.

Mbali na suala la Lugha lakini pia aliwahasa wasanii wa Filamu nchini kuwa wanapaswa kuwa na uongozi mzuri utakao simamia kazi zao za sanaa na wao kuendelea kujifua kwa kazi zaidi hii itawafanya kufanikiwa zaidi katika kazi yao ya sanaaa.katika kumbukumbu za mwaka mmoja za kifo cha The Great Kanumba Meneja wake huyo aliongozana na wasanii wengine kutoka nchini mbalimbali ili kuazimisha kumbukumbu hizo na kuonesha upendo waliokuwa nao kwa Kanumba the great.


Prince Richard Nwaobi akiwa na Seth Bosco mdogo wa marehemu kanumba. 


0 comments:

Post a Comment