Wednesday, April 24, 2013

MR NICE LEVEL NYINGINE SASA

Msanii maarufu kutoka Tanzania alietamba sana na Style ya TAKEU nchini Afrika Mashariki na kuweza kufanikiwa kufanya Shows Kibao ndani na nje ya Tanzania Mr Nice hivi sasa amepata Shavu katika nchin ya Kenya kwa kufanya kazi chini ya kampuni ya GROUND PA FAMILY chini ya Msimamizi REFIGA.

Kwa mujibu wa Meneja wa MR NICE MR REFIGA ambae anameneji wasanii kama DNA,MR NICE na wasanii wengine kutoka Kenya amethibitisha kufanya kazi na Msanii Mr Nice toka Tanzania na kusema kuwa wao wanafanya kazi hivyo ikitokea kuna mtu atakuwa teyari kufanya kazi na Mr Nice kutokea GROUND PA FAMILY mILANGO ipo wazi.

Mpita Njia alifunguka na kumcheki msanii DNA tokea kenya ambae kwa sasa anafanya kazi pamoja na Mr Nice chini ya Kampuni moja ya Ground Pa Family nae alisema kuwa ni kweli kampuni yao imeamua kufanya kazi na Mr Nice japo hakutaka kufunguka mambo mengi na kutupa mwongozo wa kumcheki Boss wao ambae ni REFIGA.

Lakini kwa kumbukumbu yangu kabla ya Mr nice Kuibukia Nchini Kenya CHINI ya Usimamizi Mpya Makini wa kazi yake alikuwa na makubaliano ya kufanya kazi na Producer Lamour Kutokea Fishcrub na makubaliano yalikuwa ni kufanya ALBUM nzima baada ya muda mfupi baada ya makubaliano hayo Mr NiCE ALIACHIA Tracks kadhaa ambazo azikuweza kupenya vizuri katika soko la muziki wa Kitanzania na kuweza kumrudisha katika PICK YAKE.

Matumani yangu ni kuwa Ground PA Family wameona kuwa Mr Nice anauwezo wa juu katika kufanya muziki ndio maana wameamua kumpa dili hilo ya kusaini Mkatba Chini ya GROUND PA FAMILY hivyo tusubili mambo mazuri ya Nice akiwa katika uongozi mpya na menejimenti Mpya .

0 comments:

Post a Comment