Na Gerald Kitalima
NYOTA wa muziki wa Bongo
Fleva Dayna Nyange ambae anauwakilisha mkoa wa Morogoro katika tasnia
ya muziki amefunguka na kusema kuwa picha alizopiga na Nay wa Mitego
zimemkwaza mpenzi wake,Dayna alisema haya alipokuwa
akihojiwa katika
kipindi kimoja cha Radio (XXL cha Clouds Fm).
Mwanamuziki huyo ambaye kwa
sasa ameachia wimbo mpya unaofahamika kama 'Nitulize' anasema kuwa
picha hizo zenye utata machoni kwa watu zilipigwa kwa ajiri ya
kutengeneza Cover ya wimbo huo mpya lakini anadai kuwa alivaa nguo za
kuogea ndiyo maana katika picha hizo ameonekana kama hajavaa nguo
yoyote juu.
Ni kweli picha hizi zimenipa
shida na kunifanya kugombana na mpenzi wangu lakini nashukuru baadaye
aliweza kunielewa,unajua sikuwa na lengo la kupiga picha ya namna hii
lakini mpiga picha wetu ndiye alitoa wazo hilo hivyo Nay wa Mitego
alibidi apige kivua wazi na mimi nilikuwa nimevaa nguo ya
kuogea,hivyo mikanda ya nguo ya kuogea ilizibwa na nywele zangu ndiyo
maana haionekani na watu wanadhani nilipiga nikiwa sina nguo"
"Lakini nilivaa nguo
sema ilikuwa ni nguo ya kuogea sema kwa kuwa picha ile ilikatwa
kuanzia kiunoni kuja juu inamfanya mtu ajue kuwe huenda tulikuwa
falagha na kuhisi labda hatukuwa na nguo lakini mimi nilikuwa na nguo
na Nay wa Mitego pia alikuwa na nguo" Aliongeza Dyana.
Mbali na hilo Dyana alielezea
tetesi zilizopo kuwa huenda anatoka na msanii Roma Mkatoliki na
kusema kuwa yeye hana mahusiano ya kimapenzi na Roma ila tu Roma
amekuwa mtu wake wa karibu sana ambaye amekuwa na mchango mkubwa
katika kazi zake za sanaa na hata katika maisha ya kawaida kuwa
wamekuwa wakishauriana mambo mengi.
"Unajua Roma Mkatoliki
ni mshikaji wangu kitambo sana yaani nipo nae karibu ila sina
mahusiano naye ya kimapenzi,tumekuwa tukishauriana na kuelimishana
mambo mbalimbali kuhusu maisha hata sanaa yetu,hivyo naweza kusema
Roma anamchango mkubwa katika kazi yangu ya sanaa"
Akielezea kuhusu sanaa yake
Dyana alisema anaamini muda ukifika ataweza kufahamika na kufanya
vizuri kama wasaniii wengine ila kwa sasa hawezi kufanya kazi na
wasanii wa nje kama ambavyo wasanii wengine hufanya.
"Ni kweli mimi nimeanza
muda muziki na nimekuwa nikijitahidi kufanya kazi nzuri na kutoa
video nzuri lakini siwezi kulalamika kwanini siwi msanii mkubwa
kihivyo kama wengine ila naamini kuwa muda ukifika kila kitu kitakuwa
sawa,maana siwezi kufanya muziki wa kiki ili nitambulike kila kona
ila muda ukifika nitakuwa msanii mkubwa kama wengine tu."
0 comments:
Post a Comment