Sunday, February 9, 2014

UJUMBE WA PROF JAY KUHUSU ELIMU HUU HAPA.

Mwanamuziki Prof Jay ambae kwa sasa anafanya kazi yake ya muziki huku akijihusisha na biashara mbalimbali ikiwemo Saloon na biashara ya muziki kupitia
katika studio yake ya Mwanalizombe,Prof ameonesha wazi kuwa kuna haja kubwa kwa wanafunzi kusoma sana wanapopata nafasi hiyo ili kuja kukabiliana na maisha mbele ya safari.
Mwanamuziki huyo amejaribu kutoa mfano kwa kuonesha aina ya maisha ambayo alikuwa akiishi kipindi ambacho alikuwa shuleni ambapo ameonesha hakuwa makini sana na Elimu kitu ambacho kwa sasa anakijutia na kutamani angepata nafasi toka enzi za kutambua aina ya maisha atakayokutana nayo.
Darasa la tano 'b'. ... Daftari moja masomo yote.. Tungejua yanayokuja kutokea huko mbele...Tungesoma mpaka tupate KIBIYONGO... ‪#‎ELIMU‬ KWANZA!!”
Hili liko wazi kwa viajana wengi tunapenda kupuuza Elimu na kuona kama kitu kisocho na msaada kwetu na kuhitaji maisha fulani ya haraka hali8 ambayo baadae huwa tunakuja kuijutia kwa namna moja au nyingine pindi tuonapao wenzetu ambao waliweza kuvumilia na kumshilikia Elimu jinsi ambavyo mambo yao wanakuwa wakiyaendesha.

Kwa kuliona hili tunapaswa kushirikilia Elimu na kuifanya kuwa kitu cha kwanza huku tukisubili mambo mengine ambayo yatakuja baada ya Elimu.

0 comments:

Post a Comment