Wednesday, February 12, 2014

NITAMJENGEA NYUMBA MAMA ILA SI YA MAMILIONI YA PESA-LINEX MJEDA

Mwanamuziki Linex Sunday Mjeda ambaye asili yake ni Kigoma na anafanya poa katika muziki wa Bongo fleva amefunguka na kusema kuwa kwa mwaka huu
ataanza kumjengea nyumba Mama yake mzazi ambae anaishi Kigoma.

Linex ameweka wazi mpango wake huo wa kumjengea mama yake nyumba ambayo amedai haitakuwa ya Mamilioni ya pesa ila nyumba ambayo mama yake atakumbuka kuwa Mwanae Linex ndie kamjengea kwa gharama yake kama zawadi ya kumzaa na kumlea katika mazingira magumu ya shida sanaa.

Mbali na hilo msanii huyo amekili wazi kuwa hajawahi kumfanyia Mama yake jambo lolote lile kubwa katika maisha yake na hiyo ni kutokana na ukweli kwamba alikuwa akitafuta maisha na kupambana na maisha.

Ujumbe huu umfikie mama angu sijawahi kukufanyia jambo lolote kubwa katika maisha cos mwanao nilikua napambana lakin nakuahid mama kitendo cha kunizaa mwanao siku ya wapendanao /Valentine sikulipi fadhila but mwaka huu ntastart kukujengea nyumba ambayo si ya mamilion ya pesa but nyumba ambayo utakua mwanao Sunday kakujenge kukushukuru kwa kumzaa valentine na kumlea katika mazingira magum ya shida sanaaaaaaaaa”

0 comments:

Post a Comment