Wajumbe
wa Bunge la katiba wamekataa posho ya Laki tatu ambayo ndio ilikuwa
imepangwa walipwe kila siku kwa muda wa siku 70 ambazo watakuwepo
Mjini
Dodoma kujadili juu ya Katiba,wajumbe hao baadhi wameonesha
kutokubaliana na posho iliyokuwa imepangwa awali na kuhitaji kulipwa
pesa zaidi kwa siku kwa madai kuwa posho hiyo haitoshi kuendesha
maisha ya kila siku mjini Dodoma.
Mbunge
wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe ametoa msimamo wake juu ya sakata
hilo na kusema kuwa yeye hawezi kupokea nyongeza ya posho hizokwani
kwa kufanya hivyo nae atakuwa katika kundi la walafi ambo yeye
amewaona hawana maana.
“Naomba
niseme wazi kabisa kwamba, sitapokea nyongeza yeyote ya posho hata
ikiongezwa. Inaweza isisaidie kuzuia walafi wengine kupata posho
kubwa lakini ni bora kuhesabika kwamba nimesema hapana. Ifikie wakati
tuseme hapana kwa excesses zisizo na maana.
Ninamwomba
Rais asikubali kuongeza posho kama baadhi ya wajumbe wa BM
wanavyotaka. Wanachopata kinawatosha sana. Nawasihi wananchi mumwombe
na ikibidi kumshinikiza Rais kukataa.”
Nae
msanii maarufu wa miondoko ya Hip Hop nchini Mwana FA nae amefunguka
na kuonesha wazi kuwa hajapenda kitendo cha baadhi ya wajumbe wa
bunge la katiba kudai Posho zaidi ya laki tatu.
“Wabunge,laki 3
yenyewe roho zinatuuma hatujajua tu tuwafanyeje kuzuia na mnaiona
ndogo..nyie watu,kuweni serious aisee.Kama
wanaona haitoshi na wanamaanisha wajiuzulu hizo nafasi zao tujue wana
msimamo...tutawakubali sana..
”
0 comments:
Post a Comment