Monday, February 3, 2014

KALLAH JEREMIAH ANAKUJA NA ZAWADI YA VALENTINE

Msanii Kallah Jeremiah ambae ameweza kufanya vizuri kwa mwaka jana na ngoma zake mbali mbali ambazo zimefungua njia na kumuongezea heshima katika kazi zake kwa sasa amezama katika mapenzi.
Kallah anategemea kuachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la You Are Not Alone siku ya Valentine day ambao ameweza kufanya na msanii mkongwe katika game Banana Zoro pamoja na Band yake.

Kallah amezidi kufunguka na kumshukuru mungu kwa kazi zake kuweza kupokelewa vizuri na jamii kiasi cha kuweza kumpa nafasi kufany6a kazi na wasanii wakongwe katika Game kama Banana Zoro,Juma Kassim Nature na wengine ambao yupo katika mpango wa kufanya nao kazi.

Akizungumzia juu ya kazi yake hiyo itakayofuata baada ya walewale Kallah amesema wimbo huo wa You Are Not Alone utazinduliwa siku ya Valentine na utapigwa Live na Band ya B- Band ya Banana Zoro.

0 comments:

Post a Comment