Wednesday, December 11, 2013

SIKUWAHI FIKIRIA KUZAA NA AMINI-LINAH SANGA

Msanii Linah Sanga ambaye awali alishawahi kuwa katika Mahaba ya Dhati na Msanii mwenzake wa Bongo Fleva Mwinyi Mkuu amefunguka na kuweka wazi
kuwa kipindi yupo katika mahusiano na mkali wa Bongo Fleva kutoka THT Amini hakuwahi kuwaza wala kufikiri kuwa Mzazi Mwenza na mkali huyo ingawa Amini alikuwa akihitaji Mtoto .
 
Kwa mujibu wa Linah amedai kuwa alipokuwa katika uhusiano wa awali hakuwaza kama anaweza kuwa mama 
 
Nilipokuwa katika uhusiano wangu wa kwanza hakuna hata siku moja niliyohisi kama nitakuja kutamani kupata mtoto maana mwenzangu aliponiambia tuzae nilimkatalia tofauti na leo hii natamani nishike mimba na ulimwengu wote ujue kwamba nina mimba,”

Linah Sanga ambaye kwa sasa walishawekana kando na Amini hajaweza kuweka wazi mahusiano yake ya sasa ambayo inaonesha kumchanganya kiasi cha kuhitaji kuwa Mzazi wa huyo mchumba wake wa sasa tofauti na ilivyokuwa kwa Mkali wa Masauti Mwinyi Mkuu.

0 comments:

Post a Comment