Tuesday, December 10, 2013

SAJUKI BADO ANAMTESA WASTARA

Baada ya kuwa kimya muda mrefu kwa kuondokewa na mumewe (Sajuki) , Wastara leo kupitia Mitandao ya Kijamii amefunguka ya
moyoni kuwaomba watanzania wamuombee aliyekuwa mumewe Marehemu Sajuki aliyefariki mwaka jana Tarehe 2 January.


“Siku week mwezi hatimae mwaka unaingia tokea ukimbie mikononi mwangu mwetu, milele nitakukmbuka daima nahisi uko sehemu nzuri unanisubiri, tal 2/1/2014 my bld anatimiza mwaka tokea atutoke katika hii dunia, nawaomba tuwe pamoja katika duwa itakayofanyika mkoani songea kokote ulipo inua mikono kumuombea juma kilowoko aka sajuki and mboni ya wastara”


Ni wazi kuwa Wawili hawa walipendana kwa dhati huku kila mmoja akiwa na imani na mwenzake kwa asilimia zote ndio maana miaka itapita lakini kumbukumbu ya Juma Kilowoki haiwezi kufutika kwa wepesi kwa Wastara kutokana na ukweli kwamba Sajuki alikuwa na mapenzi ya dhati kwa mkewe huyo ambayo kwa namna moja au nyingine wamepitia naye magumu mengi ambayo yapo tuliyoyashuhudia.

0 comments:

Post a Comment