Tuesday, December 10, 2013

MANJI AMTAMBULISHA RASMI BENO KATIBU MKUU YANGA

Mwenyekiti wa Young Africans Yusuf Manji leo amemtambulisha rasmi Bw. Beno Njovu kuwa katibu mkuu mpya wa klabu akichukua nafasi ya Lawrence
Mwalusako aliyekua kaimu katibu mkuu kwa kipindi cha mwaka mmoja.
 
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga, Mwenyekiti wa Yanga Bw.Yusuf Manji amesema Beno Njovu anaanza kuitumikia hiyo nafasi mpya kuanzia leo na Mwalusako atakua nae pamoja kwa kipindi cha mwezi mmoja mpaka atakapokabidhi kazi rasmi.

Aidha Manji ametangaza mkutano mkuu wa wanachama Januari 19,2013 ambapo wanachama watapata fursa ya kupitia mapato na matumizi, na ajenda zingine mbalimbali ambazo zitajadiliwa katika mkutano huo.

Kikao cha kamati ya utendaji kilichoketi mwishoni mwa wiki kimemteua Bw.Seif Ahmed "Magari" kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Kimataifa na kutokana na nafasi hiyo pia ameteuliwa kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Utendaji wa klabu ya Yanga.






0 comments:

Post a Comment