Tuesday, December 17, 2013

RAMA DEE AELEZA SABABU KUCHELEWA KWA VIDEO KAMA HUWEZI

Msanii Rama Dee ambaye kwa sasa anaishi Nchini Australia amefunguka na kusema kuwa Majukumu ya shule ndio sababu ya yeye kuchelewa kufanya Video
ya Wimbo wake Kama Huwezi ambao umefanya vizuri katika Radio Station mbalimbali Tanzania.

Nimechelewa kufanya Video ya Kama huwezi kutokana Na majukumu ya kimasomo naomba tuwe Na subira Ndugu zangu hiyo ndio sababu ya msingi”

Kama huwezi ni Wimbo uliotoka Katikati ya mwaka huku akiwa amempa shavu Mwanadada LadyJaydee na kuweza kupenya katika kila kona kutokana na umahiri wa wakali hao wawili walioshirikiana vizuri kutengeneza kitu kizuri na kuwakonga nyonyo Watanzania.

Lakini licha ya Kusongwa na masuala ya shule Rama Dee ameeleza kuwa hivi karibuni ataanza tena kufanya kazi za sanaa kwa kuwa atapata muda wa kufanya hivyo.

Ratiba yangu ya kufanya mziki itaanza tena karibuni...Mipango ya kuifanya video ya Kama Huwezi niliisimamisha kutokana na majukumu ya shule”



0 comments:

Post a Comment