Tuesday, December 17, 2013

BAADA YA OKWI KUTUA YANGA NIYONZIMA AFUNGUKA

Kiungo Mshambuliaji wa Yanga Haruna Niyonzima 'Fabregas' amefunguka na kusifu uongozi wa Yanga Kumuongeza Mchezaji Emmanuel Okwi katika kikosi cha
'Wanajangwani',Mshambuliaji huyo amekili na kufurahi kuongezewa nguvu ya wachezaji matata ambao kwa pamoja wanaunda Kikosi cha Jangwani.

"Siamini kama kweli Okwi ametua Yanga, ni usajili makini kwa ajili ya mafanikio ya timu hasa katika mashindano ya kimataifa. Yanga itatisha kwa sababu sasa imekamilika kila idara," alisema Niyonzima ambaye jana ndiyo ilikuwa siku yake ya kwanza kujifua na kikosi cha kocha Mholanzi Ernie Brandts tangu arejee akitokea kwenye mashindano ya Kombe la Chalenji.



0 comments:

Post a Comment