Mshambuliaji mpya wa
mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Yanga, Mganda
Emmanuel Okwi, amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuichezea klabu
Yanga kwa thamani ya shilingi milioni 355.2 za Tanzania.
Okwi
ambaye amewahi kuichezea Simba kabla ya klabu hiyo kumuuza Etoile du
Sahel ya Tunisia kwa Dola 3,000 za Kimarekani sawa na Sh. milioni 480
za Tanzania ambazo hata hivyo hadi leo Wekundu wa Msimbazi hao
wanadai hawajalipwa, Yanga imeipata saini yake kwa kiasi cha Dola za
Marekani 150,000 sawa na Sh. milioni 240 za Tanzania.
Mbali na
dau hilo, pia atakuwa akilipwa mshahara wa Dola za Marekani 3,000
kila mwezi ambazo ni sawa na Sh. milioni 4.8 za Tanzania, huku
akipatiwa malazi na usafiri binafsi wa kutembelea.
Hivyo, Sh.
milioni 4.8 atakazozilipwa kwa mwezi zitamfanya katika mkataba wake
wa miaka miwili kuvuna jumla ya Sh. milioni 115.2 ambazo ukijumlisha
na dau lake la usajili la Sh. milioni 240, zinamfanya hadi
atakapomaliza mkataba wake wa miaka miwili, kuitumbua Yanga jumla ya
Sh. milioni 355.2.







0 comments:
Post a Comment