Friday, November 8, 2013

WASANII WA BONGO BILA UMOJA MTAENDELEA KUUMIZWA TU-HALIMA MDEE

Mbunge wa Kawe Halima Mdee amefunguka leo na kusema kuwa wasanii wa Bongo wasipokuwa na umoja katika Kazi zao za Sanaa kila siku
wataendelea kuumizwa na wajanja wachache wanaotumia sanaa kujinufaisha wenyewe kauli hiyo imetolewa na Mbunge huyo kufuatia Wasanii hao kutotilia umuhimu mambo ya msingi ambayo yanahusu sanaa zako.

Kwa mujibu wa Mdee kuna wasaniii walialikwa kwenda kushiriki kuchangia Maoni yao juu ya Sheria ya sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza (1976) lakini katika Wasanii ambao walipewa mualiko huo hakuna hata mmoja ambaye alifika kuchangia katika Ngazi ya kamati ambapo walikuwa na nafasi ya kuchangia.

Tulialika wasanii katika ngazi ya kamati waje kutoa maoni ...hawakujitokeza .

Leo wakati Wabunge wakijadili Mabadiliko ya Sheria ya Filamu na Michezo Msanii mmoja wa Filamu ambaye anafahamika kwa jina la Batuli alihoji kwanini baadhi ya wasanii hawajaonekana Bungeni ndipo alipojibiwa kuwa hata vikao vya msingi ambavyovingewapa nafasi ya kuchangia hawakuweza kutokea.

Mbunge Halima Mdee aliendelea kusema kuwa wasanii wanapaswa kuifanyia kazi changamoto waliyonayo ya Kugawanyika na wanapaswa kuwa kitu kimoja ili waweze fanikisha Mambo yao na kujikomboa katika matatizo lukuki yaliyowazunguka.


Ni changamoto ambayo inabidi muifanyie kazi. Bila umoja,mtaendelea kuumizwa!”

0 comments:

Post a Comment