Friday, November 8, 2013

WANAMBARALI WANALIA NA MWEKEZAJI ASABABISHA MAUAJI

Taarifa zilizotufikia kutoka katika vyanzo mbalimbali zimesema kuwa, wananchi wa kata ya Ubaruku wilayani Mbarali Mkoani Mbeya wamezusha mapigano ya
wenyewe kwa wenyewe kutokana na kitendo cha Walinzi wa Shamba NAFCO Mbarali kumuuwa kwa kumpiga Risasi Mtu Mmoja kwa kupita sehemu iliyozuiliwa.

Kutokana na Mapigano hayo yaliyoanza jana kufikia Leo Asubuhi zaidi ya Nyumba Tatu ziliteketezwa kwa moto na Wananchi wenye Hasira .

HAYA NI MAONI MBALIMBALI YA WANANCHI WA MBARALI JUU YA MUWEKEZAJI HUYO KATIKA SHAMBA LA NAFCO MBARALI.

SIMANZI KUBWA..."Katika hali isiyokuwa ya kawaida kumekuwa na sintofahamu ndani ya wilaya yangu ya Mbarali (Mbeya) sehemu nilipozaliwa UBARUKU ( nyumbani ) tangu eneo la shamba la mpunga ambalo lilikuwa likimilikiwa na serikali kubinafsishwa kwa mtu mmoja ambaye naweza sema ameshindwa kuliendesha shamba hilo.

Hii inatokana na migogoro ambayo imekua ikijitokeza mara kwa mara tangu kuingia kwake na baadhi ya watu wamepoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa.... ni mambo mengi sana hapo katikati yamejitokeza, wanasiasa wamefanya ya kwao lakini mwisho wa Siku Wanambarali, wananchi wa kawaida ndio tunao athirika...

kubwa zaidi ni hili ambalo limejitokeza sasa; Kwa taarifa nilizo nazon ni kwamba Jana mtu mmoja ameuawa katika eneo hilo la mwekezaji tena inavyosemekana ni kwa kupigwa Risasi na walinzi wa mwekezaji huyo, binafsi naumia sana hasa pale ambapo naona Shamba ambalo limebeba historia kubwa sana ya maisha yangu, shamba ambalo limenifanya leo hii kufikia hapa nilipo, leo hii limegeuka kuua watu wasio na hatia eti kisa amekabidhiwa mtu mmoja asiyejali utu wa wanambarali, inaniuma sana...

Nawapa pole sana wafiwa na wahanga wa vurugu zilizojitokeza na wana mbarali wenzangu kwa ujumla ambao kwa namna moja ama nyingine wameathirika kwa vurugu hizo, Nawaomba ndugu zangu wa Mbarali kuwa na Umoja, Hekima na Ushirikiano katika harakati za ukombozi wa Mbarali yetu, pia nawaombea na kuiombea Mbarali irudie enzi zake za Amani na Upendo kwa kila mtu.....Mungu ibariki Mbarali, Mungu ibariki Tanzania...




0 comments:

Post a Comment