Shirikisho la Mpira wa Miguu kupitia
kwa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura limetoa taarifa kuwa
kitendo cha Vilabu kupeleka wacheazaji wake katika Vilabu vingine
haitoi nafasi ya usajili kwa Mchezaji mwingine.
"Kama
klabu ilisajili wachezaji 30 maana yake ni kuwa, haina nafasi ya
kuongeza wachezaji. Kwa upande wa wachezaji wa kigeni (foreign
players), tunakumbusha kuwa, kuanzia msimu ujao 2014/2015 watakuwa
watatu tu badala ya watano wa sasa,"
Tamko hilo la TFF lina maana kwamba, Yanga kwa sasa tayari imeingia mikataba ya kuwasajili kipa Juma Kaseja aliyekuwa huru na kiungo Hassan Dilunga kutoka Ruvu Shooting, haitakubaliwa kumsajili mmoja wa wachezaji hao kwani tayari ilikuwa na wachezaji 29.
0 comments:
Post a Comment