Wednesday, November 6, 2013

SIMBA WADAI POLISI WALICHANGIA UHALIBIFU UWANJANI

Klabu ya Simba ambayo alipigwa faini ya kulipa gharama ya Sh Million 25 kutokana na uhalibifu wa Uwanja uliosababishwa na Mashabiki wa Simba katika
Mechi waliyocheza na Kagera Sugar Oktoba 31, mwaka huu na kutoka kwa sare ya 1-1.
Msemaji wa Simba alifunguka na kusema kuwa wameomba muda wa kufanya malipo hayo uongezwe ili wapate kufanya tasmini kama ni kweli uharibufu huo unaendana na gharama wanazotakiwa kulipa.

Mbali na hilo msemaji huyo alifunguka na kusema kuwa Kikosi cha Polisi Kilichokuwepo Uwanjani hapo siku ya Tukio nacho kilikuwa chanzo kwa kuongeza uharibifu huo kwani walipaswa kutumia njia nyingine kutuliza vurugu zilizokuwepo kwa mashabiki uwanjani hapo na si kutumia Mabomu ya Machozi ambayo ndiyo yalifanya vurugu kuongezeka maradufu.
Kwa nini askari walipiga mabomu katika jukwaa hilo na kusababisha watu wakimbie ovyo huku wakikanyaga na kuharibu viti uwanjani? Je, hapakuwa na namna nyingine ya kudhibiti vurugu hizo badala ya kutumia mabomu ya machozi?" Alihoji Kamwaga.

0 comments:

Post a Comment