Wednesday, November 6, 2013

MBEYA CITY YASAFIRI NA MASHABIKI ZAIDI YA 300 MBEYA TO DAR

Timu ya Mbeya City ambayo katika Msimamo wa Ligi Kuu Vodacom Bara ipo nafasi ya Pili huku ikiibuliza Simba na Yanga na katika msimamo wa Ligi.

Mbeya City leo anakutana na Mwenyeji wake Azam FC katika uwanja wa Chamanzi Jijini Dar es Salaam katika Mechi zinazoendelea za Ligi KUU Vodacom,Uongozi wa Mbeya City amesafiri na mashabiki zaidi ya 300 wakitokea Mbeya kuja kutoa Support kwa Timu yao ambayo ndiyo imepanda daraja na kushiriki Ligi kuu Tanzania Bara Mwaka huu.

Tumejipanga na tunauchukulia mchezo huo kwa umuhimu mkubwa kwani tumeona jijini Mbeya timu inasapoti kubwa kutoka kwa mashabiki, kwa nini ugenini tusiisapoti ndio tukajipanga na kuamua kuja Dar es Salaam ili kuhakikisha Azam anakufa  Alhamisi kwa mabao 2- 0,” alisema.

Tumekodi  mabasi 10 kwa  ajili ya mashabiki ili kuisapoti timu, tumefunga safari ya saa 12 kutoka Mbeya kuja Dar  kuishangilia timu,” alisema Mastala huku kocha wa timu hiyo, Juma Mwambusi akiahidi kupambana kiume uwanjani.



0 comments:

Post a Comment