Wakati wanafunzi wa Kidato cha Nne wakiwa wanaendelea na kufanya
mitihani yao ya mwisho Nchi nzima huku wakiwa na imani kwa kuanza
kutumia
madaraja mapya ya ufauru baada ya Wizara ya Elimu kutangaza
madaraja hayo mapya ambayo yalikuwa hayana Division 0 lakini leo
Bungeni Naibu waziri wa Elimu Philip Mulugo amekanusha taarifa
zilizotolewa na Katibu mkuu Wizara ya Elimu na kusema kuwa hakuna
Division V na Divison 0 iko palepale.
Naibu
waziri amesema kuwa ulitokea mkanganyiko katika kutoka taarifa hizo.
Awali,
Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) lilikuwa likitumia alama A, B, C,
D na F huku alama A ikianza na maksi wa asilimia 81-100, B=61-80,
C=41-60, D=21-40 na F=0-20. Aidha kulikuwapo na madaraja ya I, II,
III, IV na 0.
Kwa mujibu ya mabadiliko hayo yaliyotangazwa wiki iliyopita na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, alama zitashuka ambapo alama A itakuwa ni (75-100),B+ (60-74), B (50-59),C (40-49), D (30-39), E (20-29) na F (0-19).
Kwa mujibu ya mabadiliko hayo yaliyotangazwa wiki iliyopita na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, alama zitashuka ambapo alama A itakuwa ni (75-100),B+ (60-74), B (50-59),C (40-49), D (30-39), E (20-29) na F (0-19).







0 comments:
Post a Comment