Monday, November 18, 2013

RAGE KUMSHIKA MKONO KIBADENI

Ingawa kuna taarifa kuwa Mzunguko wa Pili wa Ligi kuu Vodacom Bara Timu ya Simba inaweza kunolewa na Kocha Patrick Phiri lakini mwenyekiti wa Simba
Ismail Aden Rage amefunguka na kusema kuwa kweli kutakuwa na mabadiliko lakini kidogo.

"Tutafanya mabadiliko kidogo, lakini Kibadeni ataendelea kuwa kocha mkuu wa Simba. 

Tumekuwa na utaratibu wa kuvunja mikataba ya makocha wetu katikati ya misimu hali ambayo imekuwa ikisababisha kuyumba kwa timu yetu. Hatuko tayari kuona makosa hayo yakijirudia,"

Timu ya Simba Imeweza kumaliza Msimu wa kwanza wa Ligi huku ikiwa imeshikilia Nafasi ya Nne Katika Ligi Nyuma ya Yanga,Azam na Mbeya City lakini mpaka msimu wa Kwanza wa Ligi unakwisha Kocha Kibadeni King hakuweza kupata Fisrt Eleven.

0 comments:

Post a Comment