Monday, November 4, 2013

KAJALA AGEUKA MBOGO AWACHANA WANAOJIFANYA WANAJUA KUONGEA JUU YA MWANAYE.

Msanii katika Tasnia ya Filamu Nchini Kajala Masanja ambaye ni Mzazi mwenzie Produza Pfunk Majani wa Bongo Records amecharuka na kugeuka Mbogo
kunako Mtandao wa Instagram kwa kufunguka ya moyoni juu ya Malezi ya Mwanaye Paula ambaye yeye anaamini kuwa anamlea vizuri na kumfunda maadili yaliyomema ingawa baadhi ya watu wamekuwa wakifunguka kuwa anamlea vibaya Mtoto wake huyo ambaye anakuwa kwa Speed ya hatari.
 
Nawashangaa sana watu wengine mnajifanya mnajua sana kuongea kuhusu mambo yasiyo wahusu kuna mzazi yoyote anataka mwanae apotee ache mambo ya kishamba unataka mtoto avae dira kwani yeye mtu mzima kama unaona namlea mtoto wangu vibaya niachie mwenyewe zaa wa kwako mlee vizuri.”

0 comments:

Post a Comment