Friday, November 8, 2013

HAKIKA BABA YANGU AMEKUFA KATIKA MAZINGIRA KUSHANGAZA SANA-BAHATI BUKUKU.

Msanii wa nyimbo za Injili Tanzania Bahati Bukuku ambaye siku za karibuni amempoteza Baba yake mzazi, ameeleza kusikitishwa na kifo
hicho cha baba yake mzazi .
 
Bahati Bukuku amedai kuwa , mzazi wake huyo amekufa kimaajabu alipokuwa amelazwa kwenye Hospitali ya Dokta Mvungi iliyopo Kinondoni jijini Dar.

Bahati alisema kuwa baba yake hakuugua ila alipata presha iliyosababishwa na mshituko uliotokana na kupewa taarifa ya mdogo wake aitwaye Gibbons kupigwa risasi.

Hakika baba yangu amekufa katika mazingira ya kushangaza sana, alipata taarifa kwamba mdogo wake Gibbons alipigwa risasi, akapata presha, akaugua ini na kuanzia hapo hakuamka tena mpaka mauti yalipomfika.
Source:Global Plublisher



0 comments:

Post a Comment