Thursday, November 7, 2013

DIAMOND PLATNUM AMEVITAJA VIPERE NNE ALIVYOKUWA NAVYO : ADAI HAWA ALIZIDIWA UJANJA NA WEMA

Mkali wa My Number 1 Diamond Platnum alikutana na waandishi wa gazeti la Michezo la MwanaSpoti alihojiwa mambo mengi kuhusu maisha yake
kabla na baada ya kuwa Maarufu. Hii ni sehemu ya Interview aliyofanya na gazeti la Mwanaspoti.
 
Diamond: Nimewahi kuwa na wapenzi wanne katika kipindi chote cha ustaa wangu na sikupenda kubadili ovyo ila wengi wao hawakuweza kutimiza haja ya moyo wangu.
Mwanaspoti: Unaweza kuwataja majina?

Diamond: Ndiyo ila wawili wanafahamika zaidi. 

Wa kwanza kabisa alikuwa anaitwa Sarah na wa pili alikuwa anaitwa Hawa yule msichana niliyeimba naye katika wimbo ‘Nitarejea’, huyu alizidiwa ujanja na Wema Sepetu ambaye naye alikuja kuondoka kwangu na baadaye nikawa na Penieli Mungilwa.
 
Mwanaspoti: Mwanamke yupi unahisi ulimpenda kuliko wote?

Diamond: Mwanamke wangu wa kwanza Sarah Sadick huyu aliniingia sana moyoni sijajua ni kwanini. 
 
Lakini nahisi huenda kwa kuwa awali alinipenda kweli kwa kuwa wakati huo sikuwa na kitu. 
 
Hata hivyo nahisi ilitokana na mimi kutokuwa bize na wakati huo sikufikiria lolote zaidi ya yeye ilitokana na kutokuwa na kazi ya kufanya. 
 
Siku hizi sina mapenzi ya kivilee, nawaza zaidi pesa na ninaihangaikia na zaidi ni muziki wangu, hili ndilo la kwanza kabisa linalonifanya niwe bize mapenzi baadaye.
























0 comments:

Post a Comment