Tuesday, October 1, 2013

UWOYA AIPIGA CHINI KAZI ILIYOMKUTANISHA NA NDIKUMANA

Msanii wa Bongo Movie ambae kwa sasa anafanya poa kunako fani ya utangazaji kwa kuwa na kipindi cha Luninga kinachojishughulisha na kusaidia jamii
hususani watu wenye mahitaji ya kuboresha nyumba zao ambazo zipo katika hali mbaya kimuonekano na zinazoweza kusababisha hata hatari kwa wakazi wa nyumba hizo.
 
Mwanadada Irene ametangaza rasmi kuachana na kazi yake ya awali ambayo kwa namna moja au nyingine ndiyo iliyomsaidia kupata mafanikio mbalimbali aliyonayo sasa ikiwemo kupata mume ambae amezaa naye mtoto mmoja ingawa inasemekana kuwa wawili hao walishakwisha tengana na kila mmoja anaendelea na maisha yake.

Sababu kubwa za Irene kuachana na kazi hiyo ni kutaka kutumia muda wake vizuri kushughulika na kipindi chake cha luninga maana kama atafanya kazi zote mbili inaweza kupunguza ufanisi wake katika kazi hizo ingawa aliongeza kuwa ameamua pia kuwaachia watu wengine ambao hawajapata nafasi na wenye malengo ya kuendelea na tasnia ya Bongo Movie kufanya kazi hiyo.

Nimeamua kuacha mambo ya movie na kuwaachia wengine, haya maamuzi nimeyafanya kama miezi sita iliyopita… Mara ya mwisho kuigiza ni zaidi ya miezi sita iliyopita ”


0 comments:

Post a Comment