Kiongozi wa Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amedai kuwa Rais Jakaya
Kikwete amepotoshwa na baadhi ya
Viongozi wake kuwa mjadala wa bunge
ulikwenda vizuri,Mbowe aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam
alipokuwa akifungua mkutano wa siku nne wa wataalam mbalimbali wa
Chadema kutoka kanda za kichama.Kwa mujibu wa Freeman Mbowe mjadala wa Bunge haukwenda vizuri na hata wabunge wa CCM hawakuweza kujadili .
baada ya wabunge wa
upinzani kuomba mwongozo na kunyimwa fursa hiyo hadi wakaamua kutoka
nje, wabunge wa CCM waliobaki ndani hawakujadili muswada badala yake
walirusha vijembe na kejeli kwa kambi ya upinzani.
“Kwa hiyo Rais anaposema mjadala wa Bunge ulikwenda vizuri ajue kwamba amepotoshwa kwa makusudi. Watu waliomweleza rais taarifa hizi ni akina Lukuvi (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge) na Wasira (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu), ambao walikuwa wanaturushia vijembe bungeni, Rais asome hansadi aone kilichojadiliwa,” .
“Kwa hiyo Rais anaposema mjadala wa Bunge ulikwenda vizuri ajue kwamba amepotoshwa kwa makusudi. Watu waliomweleza rais taarifa hizi ni akina Lukuvi (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge) na Wasira (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu), ambao walikuwa wanaturushia vijembe bungeni, Rais asome hansadi aone kilichojadiliwa,” .







0 comments:
Post a Comment