Tuesday, October 1, 2013

HII NI KAULI YA WEMA SEPETU BAADA YA KUANDAMWA KWA KUANDIKWA VIBAYA NA WAANDISHI WA HABARI.

Wema Sepetu ni kati ya Wasanii wachache Nchini wanaoongozwa kwa kuuza vichwa vya habari na kusababisha biashara ya magazeti kuwa juu pindi tu anapotokea katika Gazeti hilo kwa stori.


Mbali na kuongoza kwa kuuza kwa magazeti kwa stori ambazo muda mwingine hupikwa na waandishi kwa lengo la kufanya biashara na muda mwingine zikiwa na uhalisia,pia Wema Sepetu anaongoza kwa kuandikwa katika vyombo vya habari kwa skendo mbalimbali. 
 
Kwa mujibu wa Wema amedai kuwa kuka kimya kwake kwa mambo anayofanyiwa na waandishi hao si kama yeye ni mjinga na wao kuchukua nafasi hiyo kuendelea kumchafua pasipo na sababu,ametililika kuwa wamekuwa wakimzushia mambo mengi sana na yeye kama binadamu yanamuumiza na kumtesa pia lakini huwa anamua kupotezea tu.

Siku za karibuni mwanadada huyo alielekea Nchini China na safari yake ya china waandishi wengi waliihusisha na biashara ya madawa ya kulevya na moja ya gazeti pendwa liliibuka na kichwa cha Habari kisemacho WEMA KUNYONGWA CHINA huku likipambwa na kichwa kidogo kisemacho AOMBA WATANZANIA KUMUOMBEA huku kukiwa na Picha ya dawa za kulevya chini yake kutokana na suala hilo ndipo mwanadada alipofunguka na kusema kuwa anachukizwa sana na waandishi wa magazeti .

I jus hate waandishi wa habari wa ya mageziti ya bongo.. hususan visa nd filamu”

0 comments:

Post a Comment