Tuesday, October 8, 2013

HAYA NDIYO MASWALI 3 AMBAYO KALA JEREMIAH AMEKUWA AKIULIZWA MARA KWA MARA NA MASHABIKI WAKE.

Msanii ambaye ni mkali wa Hip Hop Bongo anayetamba na ngoma kali kwa sasa JARIBU KUJIULIZA ambayo amempa shavu msanii Mary Lucas amefubguka na
kuzungumzia maswali matatu ambayo amekuwa akiulizwa na mashabiki zake.

kuna maswali ma tatu muhimu yamekuwa yaki ulizwa sana ngoja niyajibu tena hapa

1 Umeoa au una watoto?
jibu ni sijaoa na sina watoto

2 Nini maana ya 0444 ?
jibu maana ya 0444 ni 04:44 yani saa kumi na dakika arobaini na nne ukitaka kujua maana ya huu muda nunua album ya pasaka ambayo nimezungumzia ki undani sana maana ya muda huu kwenye intro ya album hiyo

3 Kwa nini unapopost unaanza kwa kuandika herufi ndogo halafu zinazofuata ni kubwa?
jibu mimi naamini kila kitu kinaanza kidogo halafu kinakua kikubwa kwa hiyo walioanzisha uandishi wa kuanza na herufi kubwa halafu zinakuja ndogo ni wanadamu na walikuwa na sababu zao binafsi ambazo mimi sikubaliani nazo.kwangu naona walikuwa na lengo la kuupotosha ulimwengu. usipotoke tena.

0 comments:

Post a Comment