Timu
ya Yanga Jana iliwasili Jijini Mbeya kwa maandalizi ya kuzisaka point
sita muhimu lakini mpaka wanawasili jijini Mbeya Kikosi cha Yanga
kilikuwa hakina Mshambuliaji ambae ni tegemeo Mnyarwanda Haruna
Niyonzima 'Fabregas'.
Yanga mpaka sasa ina pointi nne baada ya
kucheza mechi mbili, Jumamosi itashuka kwenye Uwanja wa Sokoine
kucheza dhidi ya Mbeya City kabla ya kucheza tena Jumatano kwenye
uwanja huo dhidi ya 'maafande' Prisons.
Kwa
mujibu wa Taarifa zilizopo zinadai kuwa Niyonzima alitarajiwa
kuwasili jana Nchini akitokea Nchini Rwanda alipokwenda kuwakilisha
Timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi).lakini mpaka sasa hakuna taarifa
zozote zilizotolewa na uongozi juu ya kuchelewa kwa Mshambuliaji
huyo.
Kwa mujibu wa Historia, Niyonzima siyo mchezaji wa kwanza wa kimataifa kuchelewa kurejea katika klabu yake nchini baada ya kuruhusiwa kwenda kwao kwa muda kwa sababu mbalimbali ikiwamo ya kwenda kuzichezea timu zao za taifa.
Kwa mujibu wa Historia, Niyonzima siyo mchezaji wa kwanza wa kimataifa kuchelewa kurejea katika klabu yake nchini baada ya kuruhusiwa kwenda kwao kwa muda kwa sababu mbalimbali ikiwamo ya kwenda kuzichezea timu zao za taifa.







0 comments:
Post a Comment