Kwa
mujibu wa Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwa (Takukuru), Leonard Swai, ameiambia Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu kuwa polisi hawajafanikiwa kuwakamata na kuwa tia
mbaroni Mkuu wa..!
Kitengo cha Habari, Wizara ya Fedha, Ingiahedi
Mduma na Mkurugenzi wa Kampuni ya And- Line (2000) International,
Daniel Ukwaya, ambao wanakabiliwa na kesi ya za
ufisadi.Wakili huyo alidai kuwa upelelezi umeshakamilika na kwamba itaendelea kutajwa kwa ajili ya kusubiri washtakiwa hao kukamatwa ili waunganishwe na wenzao na kusomewa maelezo ya awali kwa pamoja.
Kwa
pamoja wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na ufujaji wa
fedha za utoaji wa matangazo na habari kwa vyombo mbalimbali vya
habari.
Wanashtakiwa pia kwa matumizi mabaya ya madaraka, mashtaka manane ya kughushi, shtaka moja la ubadhirifu na shtaka moja la kusababisha hasara ya Sh. Milioni 19.8.
Wanashtakiwa pia kwa matumizi mabaya ya madaraka, mashtaka manane ya kughushi, shtaka moja la ubadhirifu na shtaka moja la kusababisha hasara ya Sh. Milioni 19.8.







0 comments:
Post a Comment