Wednesday, September 11, 2013

TUHUMA ZA MBUNGE JOSEPH MBILINYI 'SUGU' KUMJERUHI ASKARI ZINAFANYIWA KAZI

Tuhuma zinazomkabili Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu zinafanyiwa kazi..!

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya mazungumzo na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai mkoani humu, Lissu alisema maofisa wa polisi wamesema bado wanaendelea na upelelezi na watawajulisha watakapokuwa tayari.

Lissu alisema baada ya kufika polisi na Sugu, maofisa polisi waliwaambia kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Kwa upande wake, Sugu alisema tukio hilo halitamrudisha nyuma bali ataendelea kupigania haki za wananchi wake.

Hatua hiyo imekuja baada ya Sugu kudaiwa kumjeruhi askari wa Bunge katika vurugu zilizotokea bungeni mwishoni mwa wiki iliyopita.

0 comments:

Post a Comment