Tuesday, September 10, 2013

BAADA YA DIAMOND PLATNUM SERIKALI YAMKUMBUKA MZEE NGURUMO

Zikiwa zimepita Siku kadhaa toka kutangaza kustaafu kufanya kazi ya Muziki kwa Mzee Muhidini Gurumo na kuzawadiwa Gari na msanii wa BongoFleva Diamond
Platnum Serikali nayo imekumbuka Mchango wa Mzee Gurumo katika tasnia ya muziki kwa kumkabidhi Mzee huyo Barua kama kutambua kazi aliyoifanya toka akiwa kijana.

Tukio hilo lilifanyika Nyumbani kwake hivi karibuni nyumbani kwake Makuburi, Jijini Dar es Salaam.

Katika Picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni, Bibi. Lilly Beleko kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo akimkabidhi Mzee Muhidini Gurumo barua kama ishara ya Serikali kutambua mchango wake uliotukuka katika tasnia ya Muziki nchini pamoja na kumpongeza kwa kustaafu kazi kazi hiyo.

Wanaoshuhudia nyuma ya Mkurugenzi ni Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Bw. Addo Mwasongwe na kulia pembeni ya Mzee Gurumo ni Mkewe, Bibi. Pili Said Kitwana.

0 comments:

Post a Comment