Thursday, September 5, 2013

WANAWAKE NDIO WAATHIRIKA WAKUBWA RUSHWA ZA NGONO MAOFISINI

Chama cha Majaji Wanawake kimesema kuwa katika Tanzania Rushwa ya Ngono inawaathiri sana Wanawake Maofisini kwani baadhi ya Waajiri wamekuwa...!
wakitumia Madaraka yao vibaya kuomba Rushwa ya Ngono na kuahidi kutoa ajira, kupandisha cheo, au kuongeza posho. 
 
kimesema rushwa ya ngono bado ni tatizo kubwa ambalo limeshamiri katika ofisi nyingi hapa nchini.
 
Mwenyekiti wa chama hicho, Angela Kileo alisema waathirika wakubwa wa tatizo hilo ni wanawake maofisini, viwandani, mashuleni, vyuoni, majumbani na sehemu nyingine za uzalishaji na utoaji huduma.

Licha ya vitendo hivyo kushamiri kwa kasi kubwa Maofisi lakini kumekuwa na Usiri mkubwa kwakuwa vitendo hivyo vinafanyika kwa usiri mkubwa mbali na kutowatendea haki na kuwadhalilisha wanawake, lakini pia vinawaathiri kimwili na kisaikolojia.

Kileo aliongeza kuwa, licha ya athari zinazowapata kutokana na tatizo hilo, lakini wengi wao huogopa kuripoti katika vyombo husika kwa kuhofia kupoteza ajira.



0 comments:

Post a Comment