Thursday, September 5, 2013

SITAVAA HERENI TENA -HEMEDY PHD

Msanii mkali anaetamba katika Tasnia ya BONGO Movie na Bongo Fleva Hemmedy PHD Ameweka wazi kuwa kuanzia sasa hata vaa tena Hereni katika kazi zake za Muvi kwani moja anaona amekuwa hivyo anahitaji kuonesha utofauti kati ya sasa na zamani..!


Suala la kuvaa kwa Hereni kwa Msanii Hemedy PHD lilionekana kuwakera Fans wake wengi kwani hata Siku alipokuwa akichat Live Kupitia Ukurusa wa Facebook wa #EATV Kupitia KIKAANGONI LIVE CHAT Mashabiki zake wengi walimuuliza swali hilo la yeye kuvaa Hereni na kumshauri kuwa angeacha kwani muda mwingine ilikuwa akipunguza Ufanisi wa Kazi yake ya Uigizaji katika Baadhi ya SCENE.

Walimueleza kuwa anaweza kuuvaa uhalisia lakini inapokuja suala la uvaaji wa hizo Hereni inapunguza umakini kwa matazamaji kutokana na jinsi ambavyo anakuwa amejiweka.lakini aliahidi kuwa atabadilikia siku moja na kuaachana na Uvaaji wa Hereni hizo.

Kutokana na Kusikiliza Mawazo ya Mashabiki zake Hatimaye Mwanamuziki huyo na Muigizaji ametangaza Wazi kuwa hawezi kuvaa tena Hereni hizo katika Kazi zake.

0 comments:

Post a Comment