Thursday, September 5, 2013

BAADHI YA WANACHAMA WA YANGA WAMEDAI WAZEE WA YANGA HAWANA HOJA YA MSINGI.

Baada ya baraza la wazee wa Yanga kupinga maamuzi ya uongozi wa klabu yao kumuajiri raia wa Kenya, Patrick Naggi, kuwa katibu mkuu mpya klabu hiyo wanachama wengine wa Yanga wamefunguka na kusema...! kuwa Wazee wa Klabu wanataka kuivuruga Timu na Uongozi kiujumla kwa sababu wao hawaoni kama kuna tatizo kwa Raia huyo wa Kenya kuwa Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga kwani hata Kocha na baadhi ya wachezaji si Raia wa Tanzania lakini kwa kuwa wanauwezo wa ziada ndio maana wakawepo hapo.
"Baadhi ya wazee hawa wana kawaida ya kuibua baadhi ya mambo ili waitwe na uongozi kisha wapozwe na chochote ili waache chochoko ambazo hazina msingi klabuni kwa manufaa ya klabu," alifunguka mwanachama mmoja.

Katibu Mkuu wa Baraza la Wazee wa Yanga, Yahaya Akilimali, alisema kuwa hawakubaliani na uteuzi huo wa raia wa kigeni kushika nafasi hiyo wakati wapo wazalendo wenye elimu na uwezo kwa kuiongoza Yanga na kuipa mafanikio makubwa tu.



"Ni kama wametudhalilisha, wapo vijana wetu wasomi na wenye uwezo kushika nafasi hiyo, hatukubaliani na uteuzi huu, kwa nafasi hii nyeti inahitaji mtu mwenye mapenzi na Yanga,"






0 comments:

Post a Comment