Wednesday, September 4, 2013

TAIFA STARS INAKWENDA GAMBIA IKIWA DHAIFU,NYOTA WAKE ZAIDI YA 7 HATAKWENDA

Timu ya Mpira wa Miguu ya taifa (Taifa Stars) inaondoka leo kuelekea Banjul kukabiliana na wenyeji wao Gambia katika mechi ya kuwania kufuzu fainali zijazo za Kombe la Dunia ..!
Lakini Taifa Stars inakwenda Gambia ikiwa dhaifu kwa kuwakos wachezaji nyota ya Timu hiyo zaidi ya Saba ambao huwa katika First Eleven ambao wengi wao ni Majeruhi huku Nyota wengine hawajaweza kutokea katika Kambi ya bila kuwapo kwa taarifa yoyote ile.

Kocha Kim Poulsen wa Taifa Stars aliwataja wachezaji hao aliowahitaji sana kwa mechi dhidi ya Gambia itakayochezwa Jumamosi lakini wakakosekana kutokana na sababu mbalimbali kuwa ni Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Aggrey Moris, Salum Aboubakar 'Sure Boy', Athumani Iddi 'Chuji', John Bocco na Mwinyi Kazimoto.

Pia aliwataja nyota wengine kuwa ni wachezaji wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu; ambao hadi jana mchana walikuwa hawajawasili nchini na hakukuwa na taarifa zozote rasmi kueleza sababu zilizokwamisha ujio wao.
Mbali na Hao Stars Imemkosa Mwinyi Kazimoto aliye temwa kwa utovu wa nidhamu baada ya kutoroka kambini Kipindi wakijiandaa kucheza dhidi ya Uganda .

0 comments:

Post a Comment