Wednesday, September 4, 2013

BAADA YA MWALUSAKO KUPIGWA CHINI YANGA WAZEE WA YANGA WAMEMKATAA MKENYA

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, klabu ya Yanga imemtimua madarakani aliyekuwa kaimu katibu mkuu wa Yanga Lawrance Mwalusako na kumpa nafasi hiyo aliyekuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Kampuni ya Ligi ya Soka ya Kenya (FKL), Patrick Nagi.

Habari zilizopatikana kutoka Yanga zinaeleza kuwa Mkenya huyo amepewa mkataba wa mwaka mmoja na ajira yake ilianza rasmi Septemba Mosi.

Kwa upande wake Mwalusako alisema kwamba yeye anachofahamu ni kwamba amemaliza mkataba wake wa mwaka mmoja aliopewa na hajapewa maelekezo mengine na uongozi wa klabu hiyo pia aliongeza kwamba hana tatizo lolote na viongozi wake na kwamba yuko tayari kupokea maamuzi yoyote ambayo watayafanya dhidi yake.

Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, alisema kwamba hafahamu chochote na yeye bado anamtambua Mwalusako kuwa ndiye katibu mkuu wao.

Baaada ya sakata hilo wazee wa Yanga yamemkataa Patrick Nagi kuchukua nafasi ya Mwalusako kwa kigezo kuwa hapa Tanzania kuna watu wengi wenye uwezo wa juu wa kufanya kazi hiyo na sii huyo Patrick ambaye ni raia wa Kenya.

Pia wazee hao wamemkataa Mhasibu mpya alieletwa katika Club hiyo mwenye asili ya Waraabu

0 comments:

Post a Comment