Tuesday, August 6, 2013

NYOTA YAKO LEO JUMANNE: 6/8/2013

SIMBA – LEO (JUL 24 – AUG 23)
Jumanne ya leo jitihada zako ndizo zitakazokufanya wewe kufanikiwa kirahisi, jaribu kuwa karibu na watu wa dini ili kubrilikiwa mambo yako.Kazi nyingi nzito na ahadi kibao zisizitekelezeka zinaweza kuwa kikwazo.



MASHUKE – VIRGO (AUG 24- SEPT 23)
Leo hii ni siku muhimu sana kwako kuwa muangalifu, faida utakayopata katika mambo yako isikufanye ukabweteka na kufanya dharau kwa watu wengine,ikitokea siku ya leo ukikutana na mtu ambaye hana miguu kabisa, hiyo ni dalili kuibiwa mali yako au kupoteza vitu vya thamani kubwa,

MIZANI - LIBRA (SEPT 24 – OCT 23)
Leo fanya uchunguzi wa mambo unayoyatilia mashaka, jaribu kuwa karibu na wale ambao unahisi wanaweza kukupa msaada jihadhari na vikundi visivyofaa hasa nyakati za jioni. Jaribu kuwasiliana na wataalamu ili wakusaidie.

NGE - SCORPIO (OCT 24- NOV 22)
Leo utafanikiwa baada ya kusumbuka kwa muda mrefu tumia utakachopta kutumia na wengine usiwe mbahil, lakini elewakwamba mambo yako yamo hatarini kuharibiwa na watu, unatakiwa kuwa mpole kwa muda huu ili kupisha dhahama hiyo.

MSHALE - SAGITARIUS ( NOV - DES 23)
Siku ya leo usipokuwa makini kipato chako kitapotea bila kujua na wiki hii unashauriwa kutosafiri ili kujikinga na mabalaa katika safari hizo. Jaribu kuwa muangalifu na yoyote utakayeshirikiana naye ili kuokoa kile ambacho kitasalia

MBUZI - CAPRICORN (DES 22 – JAN 20
Leo hii tafuta njia zaidi za kukusaidia, marafiki na majirani wa karibu wanaweza kutoa mchango mzuri , kuna dalili ya kufanikiwa katika mambo yako, unashauriwa kuutumia muda huu kukamilisha mambo yako uliyokuwa umeyapanga kuyafanya.

NDOO –AQUARIUS (JAN 23 – FEBR 39)
Leo ni siku mbaya kwako inaonekana shughuli zako zinaweza zikakumbwa na dosari kuna uwezekano wa kupata mkosi kazini kwako au utaletewa biashara ambayo itakuletea balaa kimaisha. Jaribu kuwa muangalifu mipango yako yote uliyoipanga hasa leo achana nayo.

SAMAKI – PISCES (FEB 20- MACH 20)
Leo hii katika biashara zako utapata faida ambayo hukuitegemea na yule rafiki yako uliyemkosea utakusamehe madhambi uliyomfanyia. Jitahidi kukutana na wakubwa zako wakusaidie kupata ushauri.

PUNDA- ARIES (MACH 23- APR 20)
Pamoja na kwamba leo inaweza kuwa siku njema kwako utapatwa na mambo ya ajabu ajabu, mambo hayo yatakushangaza usijaribu kujibishana na watu usiowajua kunaweza kutokea ugomvi mkubwa.tegemea kupata safari ya itakayokupeleka sehemu ambayo hujawahi kufika.

NG’OMBE – TAURUS (APR23 – MAY 20)
Usiendekeze mambo makubwa kwani unaweza kujikuta ukiingia kwenye matatizo na kupata hasara, upo uwezekano wa kukutwa na balaa huko uendako.kuna uwezekano wa kutokea matatizo kazini kwako au kwa mtu anayekuhusu,

MAPACHA - GEMINI (MAY 23- JUN 23)
Vikwazo havitakosa kukuandama siku ya leo unaweza kujikuta hata wale uliowategemea sana katika utekelezaji wa mambo yako nao wakakuweka kwenye wakati mgumu

KAA – CANCER (JUN 22 – JUL 23) yoendelea kukupotezea
Jumanne ya leo usisumbuke na mambo madogo madogo ambayo yanayoendelea kukupotezea mudaa ni wakati wa kuangalia mbele, uhusiano wako na mtu uliyempata hivi karibuni awe ni mpenzi au rafiki utavurugika, Unashauriwa kuwa makini na hao marafiki wapya watakaokujia siku za karibuni.

Mtabiri Maalim Hassan YahyaHussein anapatikana Dar-es-salaam kila siku Ofisini kwake Magomeni Mwembe Chai, karibu na Kituo cha Mafuta cha SOPCO (Zamani BP). Simu 0754 672464

0 comments:

Post a Comment