Tuesday, August 6, 2013

NIMECHOSWA NA UONGOZI WA TAZARA-MWAKYEMBE.


Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amefunguka na kusema kuwa amechoswa na Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) kutokana na kushindwa kufanya kazi yao ipasavyo na kushindwa kuwalipa wafanyakazi wa Shirika Hilo.


Nimechoshwa na menejimenti ya Tazara, wanashindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi halafu wanaendelea kuwapo, mna mabilioni ya fedha mnawadai watu halafu mnashindwa kukusanya,” alisema Dk. Mwakyembe.
Waziri huyo wa Uchukuzi ameipa miezi mitatu menejimenti ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara), kuwalipa wafanyakazi malimbikizo ya mishahara zaidi ya Sh. milioni 624.4 kwa wakati na wakishindwa waache kazi.

0 comments:

Post a Comment